#HABARI: Familia ya Bi. Pendo Sangiziro, mkazi wa Nyantorontoro Kata ya Nyankumbu Halmashauri na Manispaa ya Geita mkoani Geita wamelazimika kulala nje ya nyumba yao kwa siku nne mpaka sasa baada ya kuzuka kwa moto ambao chanzo chake hakijafahamika na kuunguza vitu mbalimbali, ndani ya nyumba yao kwa siku nne mfululizo hali iliyozua taharuki na kusababisha familia hiyo kuikimbia nyumba yao wakihofia kuteketea kwa moto.
Bi. Jasimini anasema moto huo umekuwa ukitokea ghafla na kuteketeza vitu na unapodhibitiwa na zima moto, unaibuka kesho yake na kuteketeza nyumba kila mara na hapa analiomba Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lifanye uchunguzi kujua chanzo cha moto huo.
Balozi wa eneo hilo pamoja majirani wanasema moto huo wa maajabu umeteketeza na nyumba zingine, katika eneo hilo kwa mtindo huo huo, hali inayotishia usalama wa wananchi wanaoishi katika mtaa huo.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Geita Mrakibu Hamisi Shabani Dawa, amesema uchunguzi wa matukio ya moto katika eneo hilo, umeanza ili kubaini chanzo cha kuteketea kwa nyumba na mali katika eneo hilo.
Powered by #MCHEZOSUPA
JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
–
Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M – Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania
Follow @itvtz @radioonetanzania
@capitaldigitaltanzania