Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan amesema amani, usalama na utulivu wa kisiasa ni miongoni mwa mambo yanayokuza uwekezaji nchini, huku akiwaonya wanaotaka kuiharibu.

Dkt Samia ameeleza leo Alhamisi Januari 9,2025 wakati akizindua hoteli ya kisasa ya Jaz Elite Aurora iliyopo, Michamvi Mkoa wa Kusini Unguja Zanzibar. Uzinduzi huo ni sehemu ya shamrashamra ya kusheherekea miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Dkt Samia ameeleza kuna kuna wawekezaji wapo wengi wanaovutiwa na hali ya amani na utulivu iliyopo Tanzania, hivyo amewataka wanaotaka kuichokonoa kuacha mara moja.

Aidha Dkt Samia amewaahidi wawekezaji wa Tanzania Bara na Zanzibar, kuwa Serikali zote mbili zitaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi ili kuwavutia zaidi.

#CloudsDigitalupdates

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *