#MZOZOIRANINAMAREKANI
Rais wa Marekani Donald Trump ameishutumu Iran kwa “kushughulikia vibaya” meli za mafuta zinazopita kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz, akisema “sio makubaliano tuliyo nayo”.
Maoni hayo yanaonyesha udhaifu wa makubaliano ya kusitisha mapigano, huku ripoti zikionyesha migongano kuhusu kile kilichojumuishwa katika makubaliano hayo.
Hili limewadia huku Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akisema serikali yake inaanza mazungumzo ya moja kwa moja na Lebanon, ikizingatia Hezbollah kuweka chini silaha zao, kundi la wanamgambo linaloungwa mkono na Iran, na kuanzisha uhusiano wa amani.
Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani alithibitisha kuwa ataandaa mkutano wiki ijayo huko Washington “kujadili mazungumzo yanayoendelea ya kusitisha mapigano na Israel na Lebanon”.
Maafisa wa Lebanon walikuwa wameomba kusitisha mapigano kabla ya mazungumzo kuanza, lakini Netanyahu alisema katika hotuba iliyofuata kwa wakazi wa kaskazini mwa Israeli: “Hakuna kusitisha mapigano nchini Lebanon.”
Baada ya mashambulizi ya Israeli kuendelea huko Lebanon Alhamisi nzima – yakilenga kile ilichokielezea kama maeneo ya kurusha roketi za Hezbollah upande wa kusini – mashambulizi yalionekana kupungua kwa muda usiku kucha katika eneo hilo.
Trump alisema katika mahojiano kwamba Israeli “itapunguza” mashambulizi yake Lebanon ili kuunga mkono mazungumzo ya amani.
#chanzobbcswahil
#StarTvUpdate

(Feed generated with FetchRSS)