Mahakama nchini Afrika Kusini, imezuia kusafirishwa nchini Zambia mabaki ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Edgar Lungu, aliyefariki dunia, miezi 10 iliyopita.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Hatua hii ya Mahakama, inakwamisha tena, mipango ya serikali ya Zambia kumpa mazishi ya kitaifa kiongozi huyo wa zamani, ambaye kabla ya kifo chake, alikuwa kwenye mvutano mkali na rais wa sasa Haikaide Hichilema.

Lungu alifariki dunia tarehe 5 mwezi Juni mwaka uliopita, na familia yake imekuwa ikitaka azikwe nchini Afrika Kusini, alikofia, lakini serikali ya Zambia inasisitiza kuwa ni lazima azikwe katika nchi aliyoiongoza.

Familia ya Lungu ilikwenda kwenye Mahakama Kuu jijini Pretoria kuweka zuio la mwili wake kurejeshwa nchini Zambia, baada ya mwanasheria mkuu wa serikali ya Afrika Kusini Mulilo Kabesha, kusema kuwa Mahakama ilikuwa imetoa mabaki ya kiongozi huyo wa zamani kwa serikali ya Afrika Kusini baada ya familia yake kushindwa kukataa rufaa.

Licha ya kuzuia kusafirishwa kwa mwili wa Lungu, Mahakama pia imeagiza kuwa urejeshwe kwenye chumba cha kuhfadhi maiti binafsi au sehemu nyingine itakayoamuliwa na familia, katika agizo ambalo litatekelezwa hadi Mei tarehe 21.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *