
Katika shambulio hilo kubwa la hivi karibuni zaidi lililolenga mfumo wa nishati wakati majira ya baridi yanakaribia, umeme ulikatizwa katika mikoa tisa na takriban watumiaji 854,000 walikosa umeme kwa muda kote nchini humo.
Waziri mkuu wa Ukraine amesema tukio hilo ni moja ya mashambulizi mabaya zaidi kuwahi kutokea.
Hasara ya shambulizi la Urusi Kyiv
Kusini mashariki mwa Ukraine, mtoto wa miaka saba aliuawa wakati nyumba yao ilipolengwa na takriban watu wasiopungua 20 walijeruhiwa.
Mjini Kyiv, jengo la ghorofa katikati mwa jiji pia liliharibiwa kwa kombora.
.